KWA MAOMBI NA USHAURI WASILIANA NASI KWA SIMU: +255 718 267 171 / +255 784 367 826 au +255 754 367 826. P.O.Box 71415 KARIBU SANA.

Tuesday, August 7, 2012

MAKAMU MKURUGENZI WA W.W.I MCHUNGAJI NYANDA AAGWA LEO TEMEKE

Kanisa la Evangelistic Assemblies Of God Tanzania limeondokewa na Makamu Mkurugenzi wa WANAWAKE WA INJILI (W.W.I) TAIFA Marehemu Mchungaji Mrs Juliana Nyanda katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, akizungumza katika Ibada ya kuuaga mwili wa marehemu Askofu wa Nicodemus Nyenye amesema Hakika Marehemu alikuwa ni Mwanamke Shujaa katika kazi ya Injili hasa kulingana na KAnisa lilipotoka na Mchango wa Marehemu kuwa Mkubwa.

Askofu Nyenye amezungumza maneno hayo katika Kanisa la EAGT Temeke jijini Dar es Salaam ambapo Ibada ya Kuuaga Mwili marehemu mama Nyanda ilipofanyika kabla ya kuupeleka mwili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa tayari kwa Safari ya Kuelekea Nyumbani kwake Jijinin Mwanza.

Katika Picha ni baadhi ya Matukio yaliyojiri katika Msiba huo.

 Picha ya Juu Gari Maalumu iliyokuwa imebea mwili wa Mama Nyanda ikiingia ndani ya Kanisa la EAGT Temeke.
 Picha ya juu ni Viongozi wa WWI Taifa wakishuhudia mwili wa Mama Nyanda unavyowasili katika viwanja vya Kanisa la EAGT Temeke.
 Picha ya juu ni Wachungaji wakiwa tayari kuupokea Mwili mama Nyanda tokea Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Picha juu ni Wachungaji wakiwa wameubeba mwili wa Mama Nyanda tayari kwa kuuweka katika Sehemu ya Ibada.
Picha juu ni Viongozi mbalimbali wakishauriana namna ya kuendesha mambo kabla ya ibada kuanza katika viwanja vya EAGT Temeke.
 Picha ya juu ni viongozi wa EAGT wakiwa katika Hali ya Majonzi wakishuudia namna Mambo yalivyokuwa yakiendelea kabla ya Ibada kuanza.
Picha ya juu ni Familia ya Marehemu Nyanda ikiwasili katika viwanja vya kanisa la EAGT Temeke hii leo.
Picha ya juuni Askofu Nicodemus Nyenye akiendesha ibada katika Viwanja vya kanisa la EAGT Temeke hii leo.
 Picha ya juu ni Mkurugenzi wa WWI Taifa Mama Benjamin akieleza namna alivyoweza kufanya kazi na Mama Nyanda wakati wa Uhai wake.
 Picha ya juu ni Mmoja wa wanafamilia akitoa wasifu wa Marehemu Mama Nyanda kabla ya Kuaga mwili wa Mama Nyanda.
Picha ya juu ni Mama ambaye hatukupata jina lake alitambulishwa na familia kuwa ndiye aliyekaa na Marehemu Mama Nyanda wakati wote wa Kuugua kwake.
 Picha ya juu ni Mkurugenzi wa WWI Mama Benjamin akiwa na wanafamilia wakilifungua Jeneza na kuweka mambo sawa tayari kwa Kuaga kwa wageni waliofika.
 Picha ya juu ni Baadhi ya waombolezaji waliofika katika Msiba wa Mama Nyanda hii leo katika viwanja vya Kanisa la EAGT Temeke.

No comments:

Post a Comment