KWA MAOMBI NA USHAURI WASILIANA NASI KWA SIMU: +255 718 267 171 / +255 784 367 826 au +255 754 367 826. P.O.Box 71415 KARIBU SANA.

Tuesday, October 16, 2012

JE! SPIKA MAKINDA NI MGONJWA ?.


Spika wa Tanzania Anne Makinda

Kumeanza kuwa na uvumi ambao bado haujathibitishwa rasmi na mamlaka za Serikali ya Tanzania kuhusu Afya ya Spika wa Tanzania Anne Makinda kwamba ni mgonjwa au la baada ya kuwepo habari kwamba amekwenda nchini  India kwa shuguli kikazi lakini pia  kwa ajili ya matibabu ya kawaida ya kucheki afya yake.

Tayari gazeti la Tanzania Daima la Tanzania leo limechapisha habari kwamba afya ya Spika huyo wa kwanza mwanamke nchini Tanzania inazua utata katika habari yenye kichwa cha habari  'AFYA YA SPIKA YAZUA UTATA" na kwamba huenda amelezwa katika hosptali ya Apollo nchini India.

Soma habari kamili hapa chini kama ilivyoandikwa na gazeti la Tanzania Daima la leo Jumanne 16 October 2012

No comments:

Post a Comment