KWA MAOMBI NA USHAURI WASILIANA NASI KWA SIMU: +255 718 267 171 / +255 784 367 826 au +255 754 367 826. P.O.Box 71415 KARIBU SANA.

Sunday, December 2, 2012

RAIS KIKWETE A REJEA NCHINI BAADA YA KUHUDHURIA KIKAO CHA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI JIJINI NAIROBI, KENYA


Rais Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi wenzie wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakishuhudia utiwaji saini mkataba wa haja ya kuwepo kwa ushirikiano wa kibiashara kati ya Marekani na nchi za Jumuiya hiyo katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi, Kenya.
Zoezi hili lilifanywa baina ya Mawaziri wa Bishara wa nchi wanachama wa Jumuiya na Kaimu Waziri wa Bishara wa Marekani Bi Rebecca Blank aliyehudhuria kikao hicho.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akishuhudia Rais Mwai Kibaki wa Kenya akimkabidhi nyundo Rais Yoweri Muzeveni kama ishara ya kukabidhi Uienyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi, Kenya.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika picha ya pamoja na viongozi wenzie wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Ujumbe wa Tanzania katika mkutano wa nne wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi,
Kenya.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza kijana Joel Adagson Mwigomole kwa kuibuka mshindi wa pili wa kuandika Insha kwa wanafunzi wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakati wa mkutano wa nne wa Jumuiya hiyo katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi, Kenya. Joel ni mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule ya sekondari ya Mzumbe, Morogoro.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais Yoweri Museveni wa Uganda akimpongeza kijana Joel Adagson Mwigomole kwa kuibuka mshindi wa pili wa kuandika Insha kwa wanafunzi wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakati wa mkutano wa nne wa Jumuiya hiyo katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi, Kenya.Joel ni mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule ya sekondari ya Mzumbe, Morogoro.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika picha ya pamoja na viongozi wenzie wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na washiriki mwishoni mwa kikao cha nne cha Jumuiya nje ya Jengo la Mikutano wa Kimataifa la Jomo Kenyatta jijini Nairobi, Kenya.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiagwa kwa heshima wakati anaondoka jijini Nairobi, Kenya.PICHA NA IKULU.

No comments:

Post a Comment