. Asema Wapinzani si maadui wa CCM
. Auliza mbona wenzake wamekuwa wakikutana na CHADEMA?
![]() |
Waziri Mkuu Mstaafu Frederick Sumaye akiongea na Waandishi wa Habari hapo jana |
Hatimaye Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye hapo jana alijitokeza hadharani na kuzunguza na waandishi wa habari huku akikanusha vikali kukutana na viongozi wa CHADEMA kufanya mazungumzo ya kutaka kuhamia chama hicho.
Sumaye amesema hajawi kukutana na viongozi wa chama hicho wala chama chochote cha upinzani.
Hata hivyo alisema ni makosa kufikiri vyama Upinzani na viogozi wake ni maadui wa chama tawala Chama Cha Mapinduzi,CCM
Amesema kama angekutana nao asingeficha na wala asingeogopa kuweka mambo hadharani asingekuwa wa kwanza kufanya hivyo kwa sababu anafahamu hata wenzake wanaotaka kuwania urais kupitia Chama cha Mapinduzi wamekuwa wakikutana na viongozi CHADEMA kufanya nao mazungumzo.
“Mimi ningekuwa nimekutana nao ningesema tu mbona hata hao wengine wanaoutafuta urais kwa udi na uvumba huwa wanakutana nao? Amesema Sumaye.
Alisema yeye ni mwanachama mwaminifu wa CCM na kwamba alishawahi kusema kuwa hayuko kwa ajili ya cheo na wala kukosa ujumbe wa NEC na hasa kwa njia iliyotumika hakumnyimi usingizi wala hahuzuniki kugombea urais kwa tiketi ya CCM endapo ataamua kufanya hivyo.
No comments:
Post a Comment